Sunday, December 7, 2025
spot_img
HomeHabariViongozi wa dini Mwanza watoa wito wa amani na ushiriki Uchaguzi Mkuu

Viongozi wa dini Mwanza watoa wito wa amani na ushiriki Uchaguzi Mkuu

Viongozi wa Kikristo mkoani Mwanza wamewahakikishia waumini na wananchi wote kuendelea kufurahia amani na utulivu kuelekea Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, huku wakisisitiza umuhimu wa kila mtu kutumia haki yake ya kupiga kura.

Akizungumza katika kikao kilichowakutanisha viongozi mbalimbali wa makanisa, Mwenyekiti wa Baraza la Makanisa Mwanza, Askofu Josephat Magumba, alisema anaamini uchaguzi utafanyika kwa amani kwa kuwa taifa lipo mikononi mwa Mungu.

“Kanisa likisimama mbele, kila kitu kinaenda sawa. Tunaamini hakutakuwa na vurugu. Tutaendelea kuombea nchi na kuwafundisha watu wetu kulinda amani, rasilimali na uchumi wa taifa. Hivyo waumini wajitokeze kwa wingi kupiga kura kwa kuwa ni haki yao,” alisema Askofu Magumba.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Baraza hilo, Mchungaji Lugayila Abel, alisema viongozi wa dini wana ushawishi mkubwa katika jamii, hivyo ni jukumu lao kuhimiza amani na umoja hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi.

RELATED ARTICLES

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

- Advertisment -
NMB Tanzania

Most Popular

Recent Comments