Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan, ameonekana katika matukio mbalimbali ya picha aliposhiriki Kongamano la Amani kuelekea Uchaguzi Mkuu, lililoandaliwa na Umoja wa Maimamu Tanzania (UMATA).

Kongamano hilo limefanyika leo, Agosti 24, 2025, katika Ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam, likilenga kuhamasisha mshikamano wa kitaifa na kudumisha amani kuelekea uchaguzi mkuu.










