Monday, March 9, 2026
spot_img
HomeBiasharaSHIKUHA yamteua Godwin Mpinga kuimarisha elimu na operesheni taifa

SHIKUHA yamteua Godwin Mpinga kuimarisha elimu na operesheni taifa

SHIRIKA la Kutetea Haki za Abiria Tanzania (SHIKUHA) limeongeza nguvu kwenye safu ya uongozi ngazi ya taifa kwa kumteua mkurugenzi wa shirika hilo Kanda ya Kaskazini, Godwin Mpinga kuwa Naibu Mkurugenzi wa Elimu na Opereshen Taifa.

Akizungumzia uteuzi huo, Katibu Mkuu wa SHIKUHA, Hashim Omary amesema Mpinga ataendelea kushikilia nafasi ya zamani ili azidi kuboresha ya usafiri was abiria katika kanda hiyo.

“Mpinga ni kiongozi mchapa kazi na mwenye maono, aliyeongoza vema kama Mkurugenzi wa Kanda ya Kaskazini nafasi ambayo ataendelea kushikilia ili kuemdeleza miradi na huduma kwa abiria,” amesema Omary.

Omary amesema kupitia nafasi yake mpya, atakuwa mstari wa mbele katika kuratibu na kusimamia elimu kwa abiria, kuendeleza andaa programu za mafunzo.
“Lakini pia ataendesha shughuli za kila siku za SHIKUHA kitaifa.

Uongozi wa shirika unaamini uteuzi huu utaimarisha mshikamano, kuongeza ufanisi na kuhakikisha kila abiria anapata huduma na heshima anayostahili,” amesema.

Akizungumzia uteuzi hup, Mpinga amesema ataendelea kufanya kazi kwa bidii ili shirika hilo liweze kufikia malengo yake kutetea abiria.

Amesema katika usafiri Kuna changaamoto moto nyingi, ikiwamo abiria kutokuja haki zao na kujikuta wakinyanyasika.

“Kwa hiyo nitaendelea kushirikiana na viongozi wenzangu na wadau wote Ili kuzidi kuboresha huduma ya usafiri nchini,” amesema Mpinga.

RELATED ARTICLES

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

- Advertisment -
NMB Tanzania

Most Popular

Recent Comments