Thursday, April 30, 2026
spot_img
HomeHabariMtoto wa Mugabe afukuzwa Afrika Kusini

Mtoto wa Mugabe afukuzwa Afrika Kusini

Mahakama ya Afrika Kusini imeamuru Bellarmine Chatunga Mugabe mtoto wa mwisho wa aliyekuwa Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe, kulipa faini na kufukuzwa nchini baada ya kupatikana na hatia ya makosa ya uhamiaji na kumtishia mtu kwa bunduki ya kuchezea.

Mtuhumiwa huyo, Bellarmine, anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 20, alikamatwa mwezi Februari pamoja na mwanaume mwingine kufuatia tukio lililotokea katika makazi yake mjini Johannesburg, ambapo mfanyakazi mmoja alipigwa risasi na kujeruhiwa.

Wawili hao walikuwa kizuizini tangu kukamatwa kwao na walikiri makosa yao kama sehemu ya makubaliano na upande wa mashtaka. Hata hivyo, kosa la Bellarmine la kumtishia mtu kwa bunduki ya kuchezea lilielezwa kuwa ni tukio tofauti na lile la mfanyakazi kupigwa risasi.

Mahakama pia ilibainisha kuwa, pamoja na faini hiyo, hatua za kumrudisha nchini kwake zitachukuliwa baada ya taratibu za kisheria kukamilika, huku sababu kamili za ukiukwaji wa sheria za uhamiaji zikiendelea kufuatiliwa.

RELATED ARTICLES

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

- Advertisment -
NMB Tanzania

Most Popular

Recent Comments