Wednesday, December 10, 2025
spot_img
HomeMichezoNew King yapania kuichapa Uhamiaji

New King yapania kuichapa Uhamiaji

Kocha Mkuu wa New King FC, Abdulrahman Mohamed, amesema wanatarajia mchezo mgumu dhidi ya Uhamiaji FC katika Ligi Kuu Zanzibar leo kwenye Uwanja wa Mau A.

Amesema Uhamiaji ni timu yenye uzoefu, lakini New King imejipanga kwa umakini ili kufuta makosa yaliyowagharimu walipotoka sare na Zimamoto kwenye mechi iliyopita.

“Tumeongeza umakini na tumewasoma wapinzani wetu. Tunajua maeneo yao imara na mapungufu yao, tutayatumia kupata ushindi,” alisema.

Kocha huyo aliongeza kuwa watachagua mfumo utakaoendana na mpinzani, huku lengo likiwa kupata matokeo chanya kwenye mechi nne zilizobaki kukamilisha mzunguko wa kwanza.

RELATED ARTICLES

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

- Advertisment -
NMB Tanzania

Most Popular

Recent Comments