Rais Samia Suluhu Hassan, leo Agosti 13, 2026 amezindua rasmi Kituo cha Afya Kizimkazi, kilichopo Mkoa wa Kusini Unguja, pamoja na kupokea na kukabidhi gari la wagonjwa lililotolewa na Shirika la Afya Duniani (WHO).
Uzinduzi huo ni sehemu ya miradi ya maendeleo inayozinduliwa wakati wa Tamasha la Kizimkazi 2026, lililoanza Agosti 12 na linatarajiwa kufikia kilele Agosti 14, 2026.








