Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewateua Dorothy Onesphoro Gwajima, Balozi Mahmoud Thabit Kombo na Balozi Dk. Bashiru Ally Kakurwa kuwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Taarifa hiyo imetolewa leo November 10,2025 na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dk. Moses Kusiluka ambapo amesema wengine walioteuliwa kuwa Wabunge ni Abdullah Ali Mwinyi, Balozi Khamis Mussa Omar na Dk. Rhimo Simeon Nyansaho.




