Tuesday, May 5, 2026
spot_img
HomeHabariWanafunzi St Anne Marie Academy watoa msaada kituo cha yatima DarNa Mwandishi...

Wanafunzi St Anne Marie Academy watoa msaada kituo cha yatima DarNa Mwandishi WetuWanafunzi wa shule ya St.Anne Marie Academy wametoa msaada wa vitu mbalimbali kwenye kituo cha kulea yatima cha  CHAKUWAMA jijini Dar es Salaam.Msaada uliotolewa na wanafunzi wa kidato cha sita wa shule hiyo ni pamoja na unga, mchele, sukari, mafuta ya kula, sabuni na vifaa mbalimbali vya mahitaji ya shule.Akizungumza kwenye makabidhiano hayo, Mkuu wa shule hiyo iliyoko Mbezi Kimara kwa Msuguri, Edrick Philemon alisema kuna umuhimu kwa jamii kuwakumbuka watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu na kuwapa misaada ya aina mbalimbali.Alisema imekuwa kawaida kwa kila mwaka shule za St Anne Marie Academy kutoa misaada mbalimbali kwenye vituo vya yatima kama sehemu ya kurudisha shukrani kwa jamii ambayo ina mchango mkubwa kwa maendeleo ya shule hizo.Alisema watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu wanahitaji upendo wa jamii hivyo hatua ya kuwapa msaada wa vifaa vya shule na vyakula vinawapa moyo kuwa jamii iko pamoja nao.

“Umekuwa utaratibu wetu wa kila mwaka kutoa msaada kama huu kwenye vituo vya kulelea watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu na tunaomba jamii iige mfano wa St Anne Marie Academy,” alisema


“Shule yetu imekuwa ikifanya vizuri katika mitihani ya kitaifa kuanzia shule ya awali, msingi na sekondari, tunafaulisha na kuwa wa kwanza kitaifa, kiwilaya na hata kwenye kata kwa hiyo mafanikio yote haya lazima turudishe shukrani kwa jamii kwa kutoa misaada kama hii,” alisema


Alisema shule hiyo itaendelea kutoa elimu bora kwa kuhakikisha wanafunzi wake wanaendelea kufanya vizuri kwenye mitihani ya kitaifa kuanzia ngazi ya Kata.

“Tunaishukuru serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa namna ilivyoweka mazingira mazuri kwenye sekta ya elimu na kuwa karibu na wawekezaji binafsi katika elimu hali ambayo imechangia sekta ya elimu kuendelea kukua,” alisema


Mmoja wa watoto wanaolelewa kwenye kituo hicho, Edina John alishukuru wanafunzi wa St Anne Marie Academy kwa msaada huo na kuomba jamii kuiga mfano huo.

Alisema watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu wanamahitaji mengi hivyo hatua ya wanafunzi wa shule hiyo kuamua kuwapelekea msaada imewafariji na kuona kwamba jamii inawajali.

Previous article
Wanafunzi TUSIIME kufundishwa Artificial intelligence AI Na Mwandishi WetuKATIKA jitihada za kuendana na mtaala mpya wa elimu uliozinduliwa hivi karibuni na Serikali, unaojumuisha Mahili 11 yanayolenga kuendeleza ujuzi na stadi kwa wanafunzi, shule za Tusiime zimechagua program za Kompyuta kama kipaumbele chao.“Tukiwa na dira ya kuandaa wanafunzi kwa maisha ya kesho yanayotawaliwa na teknolojia, hususan katika zama hizi za akili mnemba Artificial Intelligence (AI), shule zetu za Tusiime kuanzia shule ya awali, msingi na sekondari mpaka kidato cha sita zimeanza rasmi utekelezaji wa somo la Introduction to Complete Programming kwa wanafunzi wa ngazi mbalimbali,” amesema leo Mkurugenzi wa shule hizo, Dk Albert Katagira.Alisema lengo la kuanza kufundisha program za kompyuta ni kuhakikisha kuwa wakifika kidato cha sita, kila mwanafunzi wa Tusiime awe na ujuzi mpana wa kujua program mbalimbaali za kompyuta.Dk Katagira alisema mafunzo hayo yatamwezesha mwanafunzi kujiajiri kupitia utengenezaji wa programu rahisi, kuunda vikundi vya programmer rika (peer programming groups), kushiriki kwenye miradi ya pamoja ya teknolojia na kutengeneza suluhisho za kidigitali kwa changamoto za kijamii na kiuchumi. “Kwa sasa, mafunzo ya awali yameshaanza kwa vitendo, ambapo wanafunzi wetu wa shule ya msingi tayari wanafundishwa msingi wa programming, ikiwemo kutumia lugha kama Scratch na Python (kwa baadaye),” amesema na kuongeza.“Kwa kutambua umuhimu wa ushirikiano na jamii, hususan wazazi, shule za Tusiime inatekeleza kampeni ya uhamasishaji ili kutoa uelewa kwa wazazi kuhusu faida za mahili ya Programming,” amesemaAidha, amesema shule hizo zinatoa nafasi kwa wadau mbalimbali kushirikiana nao katika safari hii ya mapinduzi ya elimu, kuandaa wanafunzi wanaoweza kuhimili ushindani wa soko la ajira la kidigitali.“Tunawaalika wazazi, wadau wa elimu na jamii kwa ujumla kuunga mkono juhudi hizi katika kuwajengea vijana wetu msingi imara wa mafanikio ya baadaye kwasababu shule za Tusiime tunajenga kizazi cha kesho chenye maarifa, ujuzi na ubunifu,” amesema Dk Katagira.
Next article
RELATED ARTICLES

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

- Advertisment -
NMB Tanzania

Most Popular

Recent Comments