Makamu wa Rais wa Yanga, Arafat Haji, amesema msimu huu timu haina kikosi cha kwanza, bali vikosi viwili imara vyenye wachezaji wa viwango sawa.
Amesema usajili mpya umeleta wachezaji zaidi ya 10, akiwemo Doumbia, Boyeli, Tshabalala na wengine, watakaotambulishwa kesho kwenye kilele cha Wiki ya Mwananchi Uwanja wa Benjamin Mkapa.
Yanga itakamilisha tamasha hilo kwa mchezo wa kimataifa dhidi ya Bandari ya Kenya. Pia ameahidi ushirikiano kwa Kocha mpya, Romain Folz, kuhakikisha timu inapata mafanikio.




