Tuesday, April 28, 2026
spot_img
HomeHabariUmoja wa Ulaya uwaunga mkono watu walioathiriwa na mafuriko

Umoja wa Ulaya uwaunga mkono watu walioathiriwa na mafuriko

Jumanne, 28 Aprili 2026 – Mwishoni mwa Machi 2026, mvua kubwa na za muda mrefu wakati wa kilele cha msimu wa mvua wa Machi hadi Mei zilisababisha mafuriko makubwa na maporomoko ya ardhi katika Mkoa wa Mbeya, Tanzania. Kujibu hali hiyo, Umoja wa Ulaya umetoa ufadhili wa kibinadamu wa euro 100,000 kusaidia jamii zilizoathirika zaidi.

Janga hilo lilitokea kati ya jioni ya tarehe 25 Machi hadi alfajiri ya tarehe 26 Machi, ambapo mvua kubwa zinazoendelea pamoja na upepo mkali zilisababisha maporomoko mengi ya ardhi na mafuriko ya ghafla. Kata zilizoathirika zaidi—Nkunga, Lupepo, Kawetele na Ikuti katika Wilaya ya Rungwe—zilishuhudia nyumba zikifukiwa na uharibifu mkubwa wa miundombinu muhimu ikiwemo barabara.

Takribani watu 600 waliopoteza makazi yao kwa sasa wanaishi katika shule za karibu na makazi ya muda. Hali hiyo imesababisha msongamano wa watu, uhaba wa maji masafi ya kunywa pamoja na huduma duni za usafi wa mazingira, hivyo kuongeza hatari ya magonjwa. Kufikia tarehe 27 Machi, takribani watu 20, wengi wao wakiwa watoto, walikuwa wamepoteza maisha, huku wengine kadhaa wakijeruhiwa.

Janga hilo limevuruga kwa kiasi kikubwa maisha na vyanzo vya mapato, hasa kwa kaya zinazotegemea kilimo, huku pia likiongeza hatari za kiafya na ulinzi, ikiwemo magonjwa yanayo sababishwa na maji machafu, malaria, na hatari zinazohusiana na ukatili wa kijinsia.

Ufadhili wa dharura wa Umoja wa Ulaya utaiwezesha shirika la Msalaba Mwekundu nchini Tanzania kutoa msaada muhimu, ikiwemo makazi, maji safi, huduma za afya, pamoja na msaada wa usafi wa mazingira na afya ya jamii. Msaada huo pia utazingatia ulinzi wa makundi yaliyo hatarini, usawa wa kijinsia na ushirikishwaji wa jamii.

Harakati hizo zinalenga kuwafikia zaidi ya watu 2,600 walioathiriwa na mafuriko na maporomoko ya ardhi katika kata sita za Wilaya za Rungwe na Kyela, zikiendelea kwa miezi mitatu hadi mwisho wa Julai 2026. Ufadhili huu ni sehemu ya mchango wa jumla wa Umoja wa Ulaya kwa Mfuko wa Dharura wa Kukabiliana na Majanga (DREF) unaosimamiwa na Shirikisho la Kimataifa la Vyama vya Msalaba Mwekundu na Hilali Nyekundu (International Federation of Red Cross and Red Crescent Societies—IRFC).

RELATED ARTICLES

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

- Advertisment -
NMB Tanzania

Most Popular

Recent Comments