Timu ya taifa ya soka kwa watu wenye ulemavu, Tembo Warriors, itaanza kampeni yake ya michuano ya Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) dhidi ya Kenya Septemba 9 jijini Bujumbura, Burundi. Kikosi hicho kinatarajiwa kuondoka nchini Septemba 7.

Msemaji wa Shirikisho la Soka kwa Watu Wenye Ulemavu (TAFF), Khalid Msabaha, alisema Tanzania imepangwa kundi B na Kenya pamoja na Uganda, huku kundi A likiwa na DRC Congo, Zambia na Burundi.
Alibainisha kuwa maandalizi yanaendelea vizuri na malengo makuu ni ubingwa, akiwashukuru Watanzania waliojitolea kuchangia timu hiyo kushiriki mashindano hayo.




