Baraza la Michezo la Taifa (BMT) limewataka wanawake kujitokeza kwa wingi kushiriki msimu wa saba wa mashindano ya riadha kwa wanawake (First Ladies Games) yatakayofanyika Novemba 28–30 jijini Dar es Salaam.
Ofisa Mawasiliano wa BMT, Najaha Bakari, amesema maandalizi yanaendelea vizuri na yatashirikisha wanariadha kutoka Tanzania Bara na Zanzibar.
Mashindano haya yanawalenga wasichana wenye umri miaka 15–18, huku semina ya waamuzi ikipangwa kufanyika Novemba 27.




